JUSTIN BIERBER AINGIA MATATANI TENA KWA MANENO YA UBAGUZI WA RANGI

Justin Bieber aonekana kwenye video nyingine akitumia maneno ya kibaguzi
Wiki hii haijamuendea vizuri mwimbaji wa Canada, Justin Bieber ambaye ameripotiwa kuonekana kwenye video nyingine akitumia maneno yenye ubaguzi wa rangi ikiwa ni siku moja baada ya kuomba radhi kwa video ya aina hiyo iliyotolewa na TMZ.
Katika video hiyo yenye dakika 45 iliyotolewa na The Sun ambayo pia ilichukuliwa wakati akiwa na umri mdogo, Bieber anasemekana kuwa alibadili mashairi ya wimbo wake wa ‘One Less Lonely Girl’ na kuuita ‘One Less Lonely Nig**’.
Chanzo kimeiambia NY Dailye News kuwa Bieber alifanya utani kuhusu kutaka kujiunga na kundi la kibaguzi lilikuwa likiwapiga vita watu weusi la Ku Klux Klan.
“Inabidi watu walilione hili. Watoto wa kawaida katika jamii hawafanyi utani wa aina hii. Analindwa na watu wa mitandao lakini kamera hazidanganyi. Huyu ni Justin halisi.”

0 Response to "JUSTIN BIERBER AINGIA MATATANI TENA KWA MANENO YA UBAGUZI WA RANGI"

Post a Comment