Muigizaji mkongwe nchini, Mzee Small Afariki Dunia

Tanzia: Mzee Small afariki duniaMuigizaji mkongwe nchini, Mzee Small Wangamba amefariki dunia usiku huu akiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili. 

Mzee Small amefariki kwa ugonjwa wa presha baada ya kuugua kwa muda mrefu kabla ya kuzidiwa jana na kupelekwa Muhimbili.

Mtoto wa marehemu aitwaye, Muhidin amethibitisha kifo cha Mzee Small. Mungu  ailaze Roho  ya  Marehemu  Mahali  pema  Peponi-Amina.
Waombolezaji wakiwa na simanzi nyumbani kwa marehemu Said Ngamba 'Mzee Small' aliyefariki usiku wa kuamkia leo katika Hospitali ya Taifa jijini Dar es Salaam.

Dada ya marehemu Mzee Small, Sauda Ngamba akiwa na majonzi baada ya kuondokewa na kaka yake.
Sauda akilia kwa uchungu.

0 Response to "Muigizaji mkongwe nchini, Mzee Small Afariki Dunia "

Post a Comment