DIAMOND PLATNUMZ ALIVYOFANYA MAKAMUZI CALIFORNIA JUMAMOSI .


Diamond Platnumz mwanamuziki wa bongo fleva asieshikika sasa hivi ambaye ni maarufu zaidi kwenye wimbo wake wa my number one aliyemshirikisha mwanamuziki mwingine wa Nigeria anayefanya vizuri sasa hivi Davido akifanya show kali jijini Los Angeles, California siku ya Jumamosi June 28, 2014 ikiwa pia akijiandaa kwenye BET award'14 inayofanyika leo jijini humo wimbo wake wa my number one aliyeshirikiana na Davido umekuwa nominated kwenye katagoli ya international collaboration. Mgeni wa heshima alikua Mhe. Ahmed Issa ambaye ni Balozi wa Heshima wa Tanzania California.
Mashabiki wa Diamond wakipagawa kwenye showa ya Diamond Platnumz iliyofanyika Los Angeles, California nchini Marekani.
 Diamond Platnumz akiwachengua mashabiki waliohudhuria showa yake ya California.
 Diamond Platnumz akishambulia jukwaa.
mashabiki wakipagawa kwa show ya kukata na shoka toka kwa rais wa wasafi Diamond Platnumz
Picha na Abdul Majid mwakilishi wa Vijimambo Los Angeles California

0 Response to "DIAMOND PLATNUMZ ALIVYOFANYA MAKAMUZI CALIFORNIA JUMAMOSI ."

Post a Comment